![]() |
Makubaliano hayo ni lazima yathibitishwe na wazazi wa pande zote mbili na serikali na Kanisa la MUNGU.
Kwanini wazazi wahusike?
Ni kwa sababu ni wazazi.
Kwanini serikali?
Ni kwasababu ni mamlaka inayoweza kumsaidia mwanandoa kupata haki zake hata kipindi mwenzi wake hayupo.
Uhusika wa serikali ni kutoa vyeti vya ndoa.
Mfano mume akifariki kisha ndugu wa mume wanamfukuza mjane na kumnyang'anya Mali, akishitaki serikalini cheti cha ndoa kitahitajika ili kumthibitisha kwamba alikuwa mke halali wa yule mwanaume.
Ndio maana serikali hutoa vyeti viwili yaani anayeolewa anapewa na anaoa anapewa.
Hata hivyo vyeti vya ndoa vina kazi nyingi pia.
Kwanini kanisa la MUNGU?
Ni kwa sababu lazima tuyafanyayo yafanyike katika Bwana YESU.
Kumbuka na sisi tu wa YESU.
Na MUNGU ndio mwanzilishi wa ndoa.
Na ndoa inahitaji ulinzi wa MUNGU na utakatifu.
Kuna mengi sana katika hilo la kwanini ni muhimu kumhusisha MUNGU kwenye ndoa.
Biblia inasema
Wakolosai 3:17 "Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana YESU, mkimshukuru MUNGU Baba kwa yeye."
Kwanini serikali?
Ni kwasababu ni mamlaka inayoweza kumsaidia mwanandoa kupata haki zake hata kipindi mwenzi wake hayupo.
Uhusika wa serikali ni kutoa vyeti vya ndoa.
Mfano mume akifariki kisha ndugu wa mume wanamfukuza mjane na kumnyang'anya Mali, akishitaki serikalini cheti cha ndoa kitahitajika ili kumthibitisha kwamba alikuwa mke halali wa yule mwanaume.
Ndio maana serikali hutoa vyeti viwili yaani anayeolewa anapewa na anaoa anapewa.
Hata hivyo vyeti vya ndoa vina kazi nyingi pia.
Kwanini kanisa la MUNGU?
Ni kwa sababu lazima tuyafanyayo yafanyike katika Bwana YESU.
Kumbuka na sisi tu wa YESU.
Na MUNGU ndio mwanzilishi wa ndoa.
Na ndoa inahitaji ulinzi wa MUNGU na utakatifu.
Kuna mengi sana katika hilo la kwanini ni muhimu kumhusisha MUNGU kwenye ndoa.
Biblia inasema
Wakolosai 3:17 "Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana YESU, mkimshukuru MUNGU Baba kwa yeye."


No comments:
Post a Comment