Tuesday, April 25, 2017

Kama MUNGU amekupa kufanya kazi yake hakikisha unaifanya kazi hiyo kwa moyo


Kama MUNGU amekupa kufanya kazi yake hakika inakupasa sana kuifanya kwa moyo na juhudi kubwa ili kuiepuka laana ya MUNGU. Kumbuka Biblia inasema amelaaniwa mtu yule aifanyaye kazi ya MUNGU kwa ulegevu.
kumbuka laana ni kitu kinachokukamata ili usiendelee.
Unaweza ukakataa kufanya kazi ya MUNGU kwa sababu tu wewe unataka kufanya biashara, lakini kila biashara utakayoifanya itakataa kwa sababu tu kuna laana ya kumgomea MUNGU kuifanya kazi yake. Dawa ni kutubu na kurudi kufanya maagizo ya MUNGU.

Ndugu, kama MUNGU amekupa kazi yake nakuomba Fanya kazi ya MUNGU kwa bidii na kwa moyo ili usiwe uliyelaaniwa.
Ubarikiwe

No comments:

Post a Comment