Saturday, December 30, 2017

NYAKATI.

Ndugu napenda kukusalimu katika jina la Yesu kristo matumaini yangu u mzima wa afya uliye dhaifu pokea uponyaji sasa.Napenda nikushirikishe ujumbe huu kwamba:
Katika nyakati zote Mungu ni mwaminifu na hawezi muacha mwenye haki wake yawezekana ulipokuwa katika wakati wa furaha,amani, kicheko au mafanikio makubwa ndipo ulihisi Mungu anakupenda ukaona Mungu yupo pamoja nawe,ngoja nikukumbushe kwamba katika hali zote Mungu yupo katika huzuni,upweke,kilio au maumivu makali Yesu yupo nawe hisi uwepo wake elewa anakupenda tena anakuwazia mema jipe moyo songa mbele usiogope,ubarikiwe.
Zaburi 34:17-19.
Na Agnes Mwasambili
0769519697.